Вход на сайт

Просмотр новости

Найдите то, что Вас интересует

Mahitaji ya huduma za moyo Comoro yaipa fursa JKCI

Дата публикации: 12-08-2026 13:04:48

Mafanikio ya kambi ya matibabu ya moyo iliyofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) nchini Comoro yamefungua fursa ya ushirikiano mpya baada ya uongozi wa Kisiwa cha Anjouan, kuomba huduma hizo ziwe zinaendelea kutolewa kupitia makubaliano ya muda mrefu.

Основное содержимое страницы с новостью.

Dar es Salaam. Mafanikio ya kambi ya matibabu ya moyo iliyofanywa na Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) nchini Comoro yamefungua fursa ya ushirikiano mpya baada ya uongozi wa Kisiwa cha Anjouan, kuomba huduma hizo ziwe zinaendelea kutolewa kupitia makubaliano ya muda mrefu.

Ombi hilo limewasilishwa leo Jumatano, Agosti 12, 2026 na Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Dk Salim Hamad, alipokutana na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dk Peter Kisenge, kujadili namna taasisi hiyo inavyoweza kuendeleza huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini humo.

Dk Hamad amesema Comoro bado haina huduma za kibingwa za matibabu ya moyo, hali inayowalazimu wagonjwa wengi kusafiri nje ya nchi kutafuta matibabu.

Balozi wa Tanzania nchini Comoro, Dk Salim Hamad (kushoto), alipokutana na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Dk Peter Kisenge, kujadili namna taasisi hiyo inavyoweza kuendeleza huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya moyo nchini Comoro.

Amesema mafanikio ya kambi ya matibabu iliyofanywa na JKCI katika Kisiwa cha Anjouan Oktoba mwaka jana yameongeza imani ya viongozi na wananchi wa Comoro kuhusu uwezo wa taasisi hiyo.

"Nilipokutana na uongozi wa Kisiwa cha Anjouan waliniomba niufikishe ujumbe kwa JKCI kuwa wanahitaji kuingia makubaliano ya kuendelea kufanya kambi za matibabu ya moyo. Hii ni hatua kubwa kwa nchi yetu katika kupeleka huduma za kibingwa nje ya mipaka yake," amesema Dk Hamad.

Kwa upande wake, Dk Kisenge amesema mwitikio mkubwa wa wananchi wakati wa kambi hiyo umeonyesha kuwa mahitaji ya huduma za moyo nchini Comoro ni makubwa, hivyo kuna umuhimu wa kuimarisha ushirikiano huo.

Amesema JKCI inaandaa mkakati wa kuongeza uelewa kuhusu huduma zake nchini Comoro ili wananchi wengi zaidi wafahamu fursa ya kupata uchunguzi na matibabu ya moyo kupitia taasisi hiyo.

"Tunataka wananchi wa Comoro wafahamu huduma tunazotoa ili wapate matibabu kwa urahisi zaidi badala ya kusafiri umbali mrefu kutafuta huduma hizi nje ya nchi yao," alisema Dk Kisenge.

Hatua hiyo inatarajiwa kuimarisha ushirikiano wa sekta ya afya kati ya Tanzania na Comoro, huku JKCI ikiendelea kupanua wigo wa utoaji wa huduma za kibingwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Visiwa vya Bahari ya Hindi.

Схожие новости

#Наименование новостиТональностьИнформативностьДата публикации
1Mashindano ya Feassa yafunga shule Morogoro Mjini, ikiibua sintofahamu01010-08-2026
2Mafanikio darasani yanaanzia kwenye afya ya mwili07.8310-08-2026
3Около 50 пациентов поступили в больницу в Коммунарке за последние сутки0012-04-2020
4Резиденты ТОР "Комсомольск" за пять лет реализовали проекты на 2,2 млрд рублей0025-06-2020
5Muhimbili yatenganisha pacha walioungana07.2310-08-2026
6В медучреждения Москвы закупили 25 новых аппаратов ЭКМО0030-08-2021
7Usalama wa kihisia msingi muhimu utekelezaji wa mtalaa05.5610-08-2026
8Еще около 90 пациентов поступили на лечение в больницу в Коммунарке0026-04-2020
9АСИ наградило компании с лучшими инклюзивными практиками0025-11-2025
10Станция скорой помощи в Москве получила 60 систем сердечно-легочной реанимации0029-01-2021

Классификация: Пресс-релизы. Схожих патентов: 0. Схожих новостей: 10. Тональность: 0. Информативность: 5.4. Источник: www.mwananchi.co.tz.